Uncategorized

ZINEDINE ATAMANI MESSI ASIONDOKE BARCELONA

admin July 5, 2020 7:47 am

ZINEDINE Zidane,  Kocha Mkuu wa Real Madrid amesema kuwa anatamani kumuona nyota wa kikosi cha Barcelona Lionel Messi anabaki ndani ya kikosi hicho ili kuongeza ushindani ndani ya La Liga. 

Mkataba wa Messi unameguka Juni 20,2021 huku ikitajwa kuwa yupo kwenye mpango wa kusepa ndani ya kikosi hicho. 

Haijafahamika kwamba iwapo Messi mwenye miaka 33 atasepa ndani ya klabu hiyo ataibukia wapi ila Manchester United ilikuwa inatajwa kuiwinda saini yake.

Zidane amesema kuwa anatamani kumuona Messi, mchezaji bora wa dunia mara sita, (Ballon d’Or) akiendelea kuitumikia Barcelona ili kuleta ushindani hasa kwa upande wao Real Madrid.

“Sijui kitu gani kitatokea mbeleni ila tuna matumaini atakuwepo ndani ya ligi hii,”.

TSHISHIMBI AFUNGUKA HATMA YAKE NDANI YA YANGA HII HAPA, HADITHI YA YANGA NA MABAO 36 YA WAZALENDO….

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply