Uncategorized

SIMBA YAJICHIMBIA KWA SASA MBEYA WAKIIVUTIA KASI NAMUNGO

admin July 28, 2020 7:47 am


UONGOZI wa Simba umesema kuwa kwa sasa wachezaji wote wapo salama wakiwa tayari kwa ajili ya mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Namungo FC unaotarajiwa kuchezwa Agosti 2.

Fainali hiyo itapigwa Uwaja wa Nelson Mandela, Sumbawanga inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote mbili.

Akizungumza na Saleh Jembe, meneja wa Simba, Patrick Rweyemamu amesema kuwa wapo Mbeya kwa sasa kabla ya kuelekea Sumbawanga kwa ajili ya mchezo huo.

“Kikosi kwa sasa kipo salama na muda huu tupo Mbeya kabla ya kuelekea Sumbawanga, kwani bado kuna siku kadhaa hapa mpaka itakapofika Agosti 2, 2020.

“Wachezaji wana morali kubwa na kila kitu kipo sawa kuelekea kwenye fainali hivyo sisi tupo tayari,” amesema.

Simba ilitinga hatua ya fainali kwa ushindi wa mabao 4-1 mbele ya Yanga huku Namungo ikishinda bao 1-0 mbele ya Sahare All Stars.

RASMI UWANJA WA TAIFA WABADILISHWA JINA SASA KUITWA UWANJA WA BENJAMIN MKAPA HUYU HAPA MRITHI WA MIKOBA YA EYMAEL YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply