Uncategorized

NYOTA WA HISPANIA ANAYETAJWA KUIBUKIA YANGA AFUNGIKIA DILI LAKE

admin August 9, 2020 7:47 am

 INAELEZWA kuwa Yanga ipo kwenye mazungumzo na kiungo wa zamani wa Azam FC na CD Tenerife ya Hispania, Farid Mussa ili kukamilisha dili lake la usajili ndani ya kikosi hicho.

Habari zinaeleza kuwa Yanga tayari wameshafanya mazungumzo na Farid Mussa kilichobaki kwa sasa ni kusaini dili jipya ili aibukie ndani ya kikosi hicho msimu ujao.

Nyota huyo ambaye yupo Bongo kwa sasa amesema;”Ni kweli nimekuwa nikitajwa kujiunga na klabu nyingi hapa Bongo hilo lipo wazi hasa kwa nyakati hizi za usajili.

“Ukweli ni kwamba kwa sasa mimi ni mchezaji huru na sehemu ambayo nitakuwa itajulikana hivi karibuni kwani uwezo huwa haujifichi na itakuwa wazi,”.

LEWANDOWSKI AYEYUSHA MATUMAINI YA CHELSEA KUTINGA ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA KOCHA LIPULI ABWAGA MANYANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply