Uncategorized

MASHABIKI YANGA WAOMBWA KUSAJILI WACHEZAJI WAWILI WA KIMATAIFA

admin August 24, 2020 9:47 am

 


UONGOZI wa Yanga umesema kuwa una wachezaji wawili wazuri wa kimataifa ambao tayari umeshazungumza nao ila unapenda kurejesha usajili wao mikononi mwa mashabiki ili waweze kuwasijili wachezaji hao.


Mwenyekiti wa Yanga, Mshindo Msolla amesema kuwa wana imani na mashabiki na wadau wa timu hiyo hasa katika masuala ya kujitolea kwa ajili ya timu yao hivyo wanaamini watafanikisha bila matatizo.

“Tunawachezaji wa kimataifa wawili ambao tayari tumeshazungumza nao kila kitu, ila tunaomba hawa gharama za usajili zifanywe na mashabiki na wadau ambao wamekuwa nasi kila wakati.


“Uwezo ninajua upo kwa sababu msimu uliopita walisajili wachezaji 10 mashabiki wenyewe ila msimu huu tunaomba waweze kusajili wachezaji wawili tu na utaratibu utatolewa hivi karibuni,” amesema.

ISHU YA KONDE BOY NA WAWA KUREJEA SIMBA IPO HIVI SENZO WA SIMBA APEWA MASUALA YA LA LIGA YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply