Uncategorized

POLISI TANZANIA YAMALIZANA NA NYOTA WATATU KWA MPIGO,MMOJA ALIKUWA ANAKIPIGA KMC

admin August 26, 2020 4:47 pm


 UONGOZI wa Polisi Tanzania, leo Agosti 26 umemalizana na nyota watatu ambao watakuwa ndani ya kikosi hicho kwa msimu wa 2020/21.

Nyota hao ni pamoja na mshambuliaji, Ramadhan Kapera aliyekuwa anakipiga ndani ya KMC yeye amesaini kandarasi ya mwaka mmoja akiwa ni mchezaji huru baada ya mkataba wake ndani ya wana Kino Boys kumeguka.

 Pia imemalizana na mlinzi wa kulia, Datus Peter ambaye alikua anakipiga ndani ya Klabu ya Mbao FC yeye amesaini mkataba wa miaka miwili akitokea Mbao FC.

Nyota wa tatu ni Kassim Shaban Haruna aliyekuwa anakipiga ndani ya Sahare ya Tanga amesaini dili la miaka miwili.
BAADA YA KUJIFUNGA KWENYE FAINALI, LUKAKU AJA NA WARAKA HUU MESSI ATAJWA KUIBUKIA INTER MILAN

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply