Uncategorized

KOCHA YANGA ATUA DAR KUMALIZANA NA MABOSI WAKE

admin August 29, 2020 6:47 am

 

ZLATKO Krmpotic Kocha Mkuu wa Yanga amewasili leo Agosti 29 Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza kukinoa kikosi hicho ambacho kilianza mazoezi Agosti 10.
Raia huyo wa Serbia anachukua mikoba ya Luc Eymael ambaye alifutwa kazi Julai 27 baada ya kutoa lugha za kiubaguzi.

Anaungana na Juma Mwambusi ambaye ni kocha msaidizi tayari alishaanza kazi ya kukinoa kikosi hicho Uwanja wa Chuo cha Sheria.

Zlatko amepewa kandarasi ya miaka miwili kukinoa kikosi hicho chenye maskani yake Jangwani na kwa sasa kinajiandaa kwa ajili ya Wiki ya Mwananchi ambapo kilele chake ni kesho Agosti 30, Uwanja wa Mkapa,
Siku hiyo ni rasmi kwa ajili ya kutambulisha wachezaji wapya na wale ambao walikuwa na kikosi kwa msimu wa 2019/20.
YANGA WASEMA WALIMTAKA CHAMA, SIMBA YAPANIA KUWAKERA,NDANI YA CHAMPIONI JUMAMOSI MESSI AINGIA ANGA ZA JUVENTUS

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply