Uncategorized

MANCHESTER UNITED WASITISHA MAZUNGUMZO YA KUIPATA SAINI YA NAHODHA WA MBWANA

admin September 3, 2020 4:47 am

 

MANCHESTER United inayonolewa na Kocha Mkuu, Ole Gunnar Solskjaer imesimamisha mazungumzo ya kumpata kiungo wa Aston Villa, Jack Grealish na kumgeukia Donny van de Beek anayekipiga Ajax.

Awali ilielezwa kuwa United walikuwa wanataka saini ya nahodha huyo wa Aston Villa anakokipiga mzawa Mbwana Samatta lakini Solskjaer amesema kuwa anataka kumtazama yule wa Ajax.

United ilikuwa tayari kuweka mezani kitita cha pauni milioni 80 kupata saini yake. Kiungo huyo aliweza kuonyesha kiwango kikubwa msimu uliopita na alikiongoza kikosi chake kujinusuru kushuka daraja.

Pia mabosi wa United walikuwa wanahitaji saini ya Jadon Sancho wa Borussia Dortmund huko dili lilikuwa gumu kwa sababu ya dau walilotajiwa kuwa kubwa.

MSERBIA AANZA NA WAWILI YANGA,SVEN APIGA MKWARA, NDANI YA SPOTI XTRA ALHAMISI KAGERE AFUNGUKIA ISHU YAKE KUDAIWA KUMPIGA SVEN

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply