Uncategorized

KESHO NI DODOMA JIJI V RUVU SHOOTING UWANJANI

admin October 1, 2020 8:47 pm

 


KESHO Oktoba 2 Ligi Kuu Tanzania Bara inaendelea kuchanja mbuga ikiwa ni raundi ya tano sasa baada ya raundi ya nne kukamilika na kushuhudia jumla ya mabao 13 yakifungwa kwenye mechi tisa zilizochezwa.


Ruvu Shooting ambayo mchezo wake uliopita ilikuwa Uwanja wa Uhuru na ililazimisha sare ya bila kufungana na Biashara United inashuka Uwanja wa Jamhuri Dodoma kumenyana na Dodoma Jiji.


Dodoma Jiji wao wametoka kupokea kichapo cha mabao 3-0 na Polisi Tanzania ambapo shujaa aliyewatungua mabao mawili Uwanja wa Ushirika Moshi alikuwa ni Marcel Kaheza nyota wa Polisi Tanzania.

Dodoma Jiji wakiwa Uwanja wa Jamhuri wamecheza mchezo mmoja ilikuwa ni dhidi ya Mwadui FC, Septemba 6 na ilishinda bao 1-0.

YANGA YADAI MKATABA WA MORRISON SIMBA SIO HALALI ISHU YA MAPUNGUFU YA MKATABA WA MORRISON, SIMBA YAJIBU KIMTINDO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply