Uncategorized

TAIFA STARS YAIVUTIA KASI BURUNDI

admin October 7, 2020 9:47 am

 


KIKOSI cha timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars kinaendelea na maandalizi ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa ulio kwenye kalenda ya Fifa.


Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Oktoba 11, Uwanja wa Mkapa ikiwa leo ni Oktoba 7 zimebaki siku tatu kabla ya mchezo kupigwa.

Kocha wa Taifa Stars, Ettiene Ndayiragije amesema kuwa maandalizi yapo vizuri na wanaamini watapata matokeo mbele ya wapinzani wao.

Nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta amesema kuwa wachezaji waliochaguliwa wapo vizuri na watapambana kupata ushindi.

“Furaha kubwa ya mashabiki ni kupata ushindi hata sisi pia wachezaji tunahitaji ushindi hivyo mashabiki watupe sapoti tutafanya vizuri,” amesema.
YANGA YACHEKELEA DABI KUPIGWA NOVEMBA 7 SIMBA YAZUNGUMZIA ISHU YA DABI KUPELEKWA MBELE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply