Uncategorized
DAVID KISSU AWEKA REKODI YAKE BONGO
DAVID Kissu Mapingano kipa namba moja wa Azam FC ameweka rekodi ya kuwa kinara wa clean sheet ndani ya Ligi Kuu Bara Bara msimu wa 2020/21.
Azam FC ikiwa imecheza mechi saba amekusanya clean sheet 6 na amefungwa mabao mawili ilikuwa dhidi ya Kagera Sugar, Uwanja wa Azam Complex wakati Azam ikishinda mabao 4-2.
Jana Oktoba 20, Azam FC ilishinda mchezo wake wa 7 kwa kuifunga mabao 2-0 Ihefu FC na kufikisha jumla ya pointi 21 ikiwa nafasi ya Kwanza Kwenye msimamo.
Kibindoni ina jumla ya pointi 21 na imefunga mabao 14 baada ya kucheza mechi zake 7
Aristica Cioaba, Kocha wa Azam FC amesema kuwa ni furaha kwa timu yake kupata ushindi kwenye mechi zao.

Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.