Uncategorized

GLOBAL FC YATUMA SALAMU E MEDIA

admin October 23, 2020 7:47 am


 KUELEKEA kwenye mechi ya kirafiki kati ya wababe wa mji Global FC dhidi ya E Media, Kocha Mkuu wa kikosi cha Global FC, Philip Nkini amesema kuwa wamejipanga kuwafunga E Media pamoja na wachezaji wao.

Leo Oktoba 23, Global FC wanatarajia kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya E Media kwenye Uwanja wa Tanganyika Packers wakiwa na kumbukumbu ya kuchapwa bao 4-1 kwenye mchezo uliopita wa kirafiki na Azam Media.

Nkini ameieleza Spoti Xtra kuwa wamejiandaa vema katika kukifunga kikosi cha E Media na kuweza kurudisha heshima kwa timu inayotumia wachezaji halali wa Kampuni ya Global.

“Ninafahamu kuwa wachezaji wengi wa E Media wanatoka nje na kufanya kikosi chao kionekane bora kuliko timu nyingine zote. Sisi tunawachezaji wa hapa hapa ndani, hawatutishi.

“Kwenye mchezo wetu uliopita changamoto kubwa ilikuwa ni kipa. Kipa wetu alikuwa safarini kwenye majukumu ila sasa amerejea rasmi. Hivyo, kwenye mechi ya kesho, kikosi cha Global kitalindwa na kipa mwenye ubora wa kimataifa,” alisema Nkini.

WANNE YANGA WAINGIA KWENYE VITA YA KUWANIA TUZO BAADA YA KUSHINDA MBELE YA POLISI TANZANIA KMC YAANZA KUIVUTIA KASI YANGA MWANZA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply