Uncategorized

VITA YA UFUNGAJI BORA MAMBO NI MOTO, AZAM YAPACHIKA WAWILI,

admin October 24, 2020 5:47 am

 


KWENYE orodha ya wafungaji Bongo nyota wa timu ya Azam FC, Prince Dube ni kinara wa kutupia akiwa nayo mabao sita na ametoa jumla ya pasi nne za mwisho.


Azam FC kwa sasa ikiwa imefunga mabao 14 yeye amehusika kwenye mabao 10 kwa kuwa amefunga mabao sita na kutoa pasi nne za mabao.

Vita yake kwenye ufungaji ni dhidi ya mshambuliaji bora wa msimu uliopita, Meddie Kagere wa Simba ambaye yeye ana mabao manne kibindoni.

Msimu uliopita Kagere alitupia mabao 22 na kutwaa tuzo ya mfungaji bora.


Pia orodha inaongezeka ndani ya Azam FC uwepo wa jina la Obrey Chirwa mwenye mabao manne ndani ya ligi na ana pasi mbili za mabao.

Pia Chris Mugalu na Bigirimana Blaise wa Namungo FC hawa wote wametupia mabao matatu matatu sawa na Kelvin Friday wa Biashara United.

Nyota mwingine mwenye mabao matatu ambaye ni mzawa anaitwa Yusuph Mhilu yeye anacheza ndani ya Klabu ya Kagera Sugar.


Meshack Abrahm wa Gwambina FC naye ni miongoni mwa washambuliaji wenye ushkaji na nyavu kwa kuwa ametupia mabao matatu.


Kwa upande wa mabeki kinara wa kutupia ni Lamine Moro wa Yanga yeye ametupia mabao mawili. 

KOCHA YANGA: MUHIMU POINTI TATU MENGINE YATAFUATA YANGA YAWASILI MWANZA, MMOJA KUWAKOSA KMC KESHO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply