Uncategorized

YANGA YA KAZE KAZINI LEO KUTESTI MITAMBO

admin November 15, 2020 7:47 am


KIKOSI cha Yanga leo Jumapili, Novemba 15 kitakuwa na kibarua cha kumenyana na African Lyon kwenye mchezo wa kirafiki.

Mchezo wa leo ambao unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Azam Complex saa 1:00 usiku ni maalumu kwa ajili ya kutesti mitambo ya timu hiyo kuelekea kwenye mechi zijazo za ligi.

 

Chini ya kocha wao Cedric Kaze raia wa Burundi,mwenye tuzo ya kocha bora Oktoba kitatoa burudani kwa mashabiki wake ambapo kiingilio ni buku tatu tu, (3,000) mzunguko na VIP ni 5,000.

 

Kambi ya Yanga ipo Kigamboni, Dar, huku ikiwa na nyota wachache kutokana na wengine kutimkia kwenye timu za taifa. Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh, amesema, kuwa: “Kila kitu kipo sawa na wachezaji wana utayari kwa ajili ya mchezo wetu wa kirafiki.

 

“Kuhusiana na mechi hiyo ya kirafiki dhidi ya African Lyon, kocha Kaze mwenyewe ndiyo ameitaka na anajua juu ya malengo yake ambayo ameyapanga kuhusiana na nini atakachokiona kwenye mechi hii.”

MSUVA: MASLAHI YAMENIPELEKA WYDAD CASABLANCA WAPINZANI WA KIMATAIFA KUTOKA NIGERIA WAANZA KUIFUATILIA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply