Uncategorized

NYOTA NGORONGORO HEROES KUWAKOSA SAUDI ARABIA

admin December 14, 2020 1:47 pm


KHELFFIN Salum Hamdoun, nyota wa timu ya taifa ya Tanzania chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes ataukosa mchezo wa leo dhidi ya Saudi Arabia baada ya kuvunjika kidole akiwa mazoezini. 


Saudi Arabia imeomba mechi ya marudiano na Ngorongoro Heroes baada ya ule wa kwanza uliochezwa hivi karibuni kushuhudia ikimaliza dakika 90 ikiwa imefungwa bao 1-0.

Kocha Mkuu wa Ngorongoro Heroes, Jamhuri Kihwelo, ‘Julio’ amesema kuwa ni mchezaji mmoja ambaye atakosekana kwenye mchezo wa leo.

“Fini ameumia kidole alipokuwa mazoezini hivyo ataukosa mchezo wa leo dhidi ya Saudi Arabia ambao ni wa marudio.

“Aliumia wakati akigombea mpira na mwenzake kwenye mazoezi hivyo hatakuwa sehemu ya kikosi kitakachocheza lakini anaendelea vizuri,” amesema.

WACHEZAJI KUTOPIMWA MATUMIZI YA BANGI VITA YA LIGI YA MABINGWA ULAYA IPO NAMNA HII

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply