Uncategorized
NYOTA YANGA AIBUKIA IHEFU FC
KIUNGO mshambuliaji wa Klabu ya Yanga Juma Mahadhi amepekwa kwa mkopo ndani ya Klabu ya Ihefu FC inayonolewa na Kocha Mkuu Zuber Katwila.
Mahadhi alirejea kikosini mwanzoni mwa msimu baada ya kuwa nje kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu akiuguza majeraha ya goti
Kutokana na ushindani wa namba kwenye kikosi cha Yanga, imekuwa changamoto kwake kupata nafasi kwa Cedri Kaze.
Meneja wa mchezaji huyo Godlisetn Anderson, amethibitisha kuwa Mahadhi ataitumikia Ihefu Fc kwa miezi sita

Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.