Uncategorized

WEST HAM UNITED YAINGIA ANGA ZA ARSENAL

admin January 9, 2021 4:47 pm

 


NYOTA wa Klabu ya Arsenal, Eddie Nketiah anatajwa kuingia Kwenye rada za Klabu ya West Ham United ambayo inahitaji kumpata mbadala wa Sebastien Haller kwa mujibu wa ripoti.


Haller ameweka rekodi ya ada ya usajili ndani ya West Ham United ambao ni pauni milioni 22 na ameibukia ndani ya Klabu ya Ajax baada ya usajili wake kukamilika Ijumaa.


Hesabu za West Ham United kuipata saini ya Nketiah mwenye miaka 21 ni pendekezo la Kocha Mkuu, David Moyes ambaye anataka kuboresha kikosi chake.


Pia kutopata namba kikosi cha kwanza ndani ya Arsenal inayonolewa na Kocha Mkuu, Mikel Arteta kunampa imani ya kumpata mchezaji huyo kwa kuwa ameanza kwenye michezo mitatu pekee ndani ya Ligi Kuu England msimu huu kutokana.

 Nafasi yake ndani ya uwanja ambayo ni ushambuliaji imekuwa na ushindani kwa nyota Alexandre Lacazette na nahodha Pierre Emerick Aubameyang ambao ni chaguo la kwanza la kocha.

KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHOANZA LEO DHIDI YA MTIBWA SUGAR NAMUNGO YAIFUNGASHIA JUMLA VIRAGO JAMHURI KOMBE LA MAPINDUZI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply