Yanga SC

HAYA HAPA MAJUKUMU MAPYA YA CARLINHOS YANGA

admin February 9, 2021 5:47 pm

 


KOCHA mkuu wa klabu ya Yanga, Cedric Kaze ameamua kumbadilishia majukumu kiungo mshambuliaji wa klabu hiyo raia wa Angola, Carlos Carlinhos kwa kumtoa katikati na kumtaka acheze kwa kutokea pembeni.

Licha ya kutumika kama namba kumi kwa muda mrefu tangu atue ndani ya kikosi cha Yanga, lakini katika mchezo uliopita wa kujipima nguvu dhidi ya African Sports uliopigwa katika uwanja wa Azam Complex Chamazi, jijini Dar es Salaam Carlinhos alionekana akicheza kutokea pembeni.

Kuhusiana na maamuzi hayo kocha Kaze amesema kupitia mbinu zake anadhani Carlinhos atakuwa bora zaidi akicheza katika eneo la pembeni, kulinganisha na katikati.

“Carlinhos katika mbinu zangu amekuwa akionyesha kiwango kizuri zaidi anapocheza akitokea pembeni kulinganisha na anapotokea eneo la katikati ya uwanja, na baada  ya kurejea nimepanga kumtumia zaidi katika eneo hilo kwa kuwa nadhani atafanya makubwa,”

AZAM WAMETUKUMBUSHA MAPUNGUFU YETU NADO: UKITAKA KUWAFUNGA SIMBA FANYA HIVI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply