Simba SC

BAADA YA KUMALIZANA NA AS VITA KITUO KINACHOFUATA NI AL AHLY

admin February 13, 2021 7:47 am


BAADA ya kikosi cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya AS Vita Club kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi, leo kinatarajiwa kuanza safari ya kurejea Bongo.

Bao pekee la ushindi kwa Simba lilipachikwa na mshambuliaji Chris Mugalu dakika ya 60 kwa mkwaju wa penalti uliosababishwa na Luis Miquissone dakika ya 59.

  Leo Februari 13 kikosi kinatarajia kuanza safari mchana ambapo kikosi pamoja na benchi la ufundi watapitia Ethiopia.

Kesho Jumapili, Februari 14 saa 6 mchana kitatua rasmi ardhi ya Bongo ili kuedelea na maandalizi ya Ligi Kuu Bara pamoja na mechi za kimataifa.

Kundi A kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika kituo kinachofuata ni Al Ahly, mchezo unaotarajiwa kuchezwa Februari 23, Uwanja wa Mkapa.


MAMLAKA YA ANGOLA YADAI KUWA WACHEZAJI WATATU NA KIONGOZI MMOJA ANA CORONA MOURINHO MAMBO MAGUMU, KUKUTANA NA GUARDIOLA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply