kimataifa

KOCHA SPURS ANATAJWA KUWEKWA KWENYE HESABU ZA KUFUTWA, ATOA KAULI YA KISHUJAA

admin February 19, 2021 3:47 pm


 JOSE Mourinho, Kocha Mkuu wa Spurs amesema kuwa licha ya mambo kuwa magumu ndani ya kikosi hicho bado hajakata tamaa.

Mreno huyo amesema kuwa wataendelea kupambana ndani ya uwanja ili kupata matokeo chanya ambayo yatawafanya warejee kwenye ubora wao wa awali.

Kwa sasa Mourinho amekuwa kwenye presha kubwa na inaaminika kwamba huenda akafutwa kazi kutokana na kutokuwa na mwendo mzuri.

“Ni ngumu lakini bado inawezekana kwetu kurejea kwenye ubora wetu na kufanya mambo yaweze kwenda sawa ndani ya uwanja.

“Licha ya kwamba Ligi Kuu England ni ngumu na kimahesabu inawezekana kuwa katika hali ya awali ndani ya uwanja,”.

Spurs ipo nafasi ya 9 kwenye msimamo na ina pointi 36 baada ya kucheza mechi 23.

POLISI TANZANIA HESABU ZAO MZUNGUKO WA PILI HIZI HAPA SIMBA WAIJIBU KIMTIDO YANGA ISHU YA KUJIONDOA KWENYE LIGI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply