kimataifa

KLOPP:ITAKUWA NGUMU KUTETEA UBINGWA

admin February 22, 2021 11:47 am


 JURGEN Klopp, Kocha Mkuu wa Liverpool amesema kuwa kwa mwendo ambao wanakwenda nao kwa sasa anaamini itakuwa ngumu kwao kutetea taji la Ligi Kuu England.

Liverpool inapita kwenye kipindi kigumu kwa sasa ndani ya uwanja kwa kuwa haipati matokeo chanya jambo linalompasua kichwa kocha huyo ambaye ni bingwa mtetezi.

Februari 22, ilikubali kichapo cha mabao 0-2 dhidi ya Everton ikiwa Uwanja wa Anfield na kuwafanya waporomoke kutoka nafasi ya nne mpaka ya sita.

Imecheza mechi 25 za Ligi Kuu England na imekusanya pointi 40 kibindoni kwa msimu wa 2020/21.

Klopp amesema:”Ligi ni ngumu na kila timu inahitaji kufanya vizuri hivyo ninaona kwamba kuna ugumu kwenye kutetea taji la ligi licha ya kwamba lolote linaweza kutokea,”.

Matokeo mabovu inayopata ni kutokana na kuwa na lundo la wachezaji wengi ambao wanasumbuliwa na majeraha ikiwa ni pamoja na beki kisiki Virgil Dijk, Fabinho.

MASAU BWIRE:PENALTI ILITUTOA MCHEZONI SIMBA YATAJA MASHINE YAO YA KAZI ITAKAYOWAPA USHINDI MBELE YA AL AHLY

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply