Yanga SC

KASEKE:TUTAIFUNGA KEN GOLD KESHO

admin February 26, 2021 12:47 pm


 DEUS Kaseke, kiungo wa Klabu ya Yanga amesema kuwa kesho wanaamini watashinda mchezo wao wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Ken Gold.

Mchezo huo utachezwa Uwanja wa Uhuru saa 10:00 jioni.

Kiungo huyo ambaye ametupia jumla ya mabao sita na pasi moja ya bao amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo huo.

“Tupo tayari kwa ajili ya mchezo wetu wa Kombe la Shirikisho na imani yetu ni kupata ushindi kwa kuwa inawezekana.

“Kikubwa ni suala la kusubiri na kuona itakuaje kwa kuwa wachezaji kiujumla wanahitaji ushindi na maandalizi yapo vizuri,” amesema.

MKUDE, YONDANI WAITWA STARS, NCHIMBI KAMA KAWA … ADAM ADAM AFIKIRIA KUCHEZA NJE YA BONGO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply