Simba SC

MFARANSA WA SIMBA LEO KUFANYA MABADILIKO MAKUBWA KIKOSI CHA KWANZA

admin February 26, 2021 12:47 pm


 IKIWA leo kikosi cha Simba kinachonolewa a Kocha Mkuu, Didier Gomes kinashuka Uwanja wa Mkapa kusaka ushindi mbele ya African Lyon, Mfaransa huyo ameweka wazi kwamba atafanya mabadiliko kwenye kikosi cha kwanza.

Mchezo wa leo ni hatua ya 32 ambapo ikiwa Simba ama African Lyon itashinda itasonga hatua ya 16 bora na ile itakayoambulia kichapo safari itakuwa imewadia.

Simba ni mabingwa watetezi ambapo waliweza kutwaa taji hili kwa ushindi wa mabao 2-0 mbele ya Namungo ambayo imetinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho, Afrika.

Wachezaji ambao wanapewa nafasi kubwa ya kupumzika leo ni pamoja na Luis Miquissone, Clatous Chama, Aishi Manula,Mohamed Hussein, Shomari Kapombe, Rarry Bwalya na Thadeo Lwanga.

Nyota hao walikuwa na kazi kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa hatua ya Makundi mbele ya Al Ahly ya Misri na walishinda bao 1-0 lililopachikwa na Luis.

Gomes amesema:”Hautakuwa mchezo mwepesi kwetu kwa kuwa kila timu inahitaji ushindi ila tutapambana kusaka matokeo chanya ndani ya uwanja.

“Mabadiliko yatakuwa makubwa kwenye kikosi cha kwanza lengo ni kuwapa mapumziko wale ambao walicheza mechi za kimataifa kwa kuwa bado tuna kaz ya kufanya kwenye mechi zijazo,” amesema.

Mchezo huo utachezwa leo majira ya saa 1:00 usiku.

ADAM ADAM AFIKIRIA KUCHEZA NJE YA BONGO KOCHA AL AHLY AONDOKA NA MAJINA YA WACHEZAJI SIMBA..ONYANO NA MIQUISSONE PIA WAMO..!!

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply