Home Simba SC SIMBA YATAJA MASHINE YAO YA KAZI ITAKAYOWAPA USHINDI MBELE YA AL AHLY

SIMBA YATAJA MASHINE YAO YA KAZI ITAKAYOWAPA USHINDI MBELE YA AL AHLY


 UONGOZI wa Simba umesema kuwa nyota wao Clatous Chama ambaye ni kiungo mshambuliaji akiwa fiti asilimia 100 timu hiyo itapata matokeo chanya mbele ya Al Ahly.

Kesho, Februari 23 Simba itakuwa na kazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Al Ahly kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa ni hatua ya makundi.

Haji Manara, Ofisa Habari wa Simba amesema kuwa kwenye kila nchi kuna mtawala na mfalme wake hivyo kwa upande wa Simba mfalme ni Chama.

“Chama akiwa bora ndani ya uwanja anaifanya timu iwe na kasi katika kusaka matokeo ambayo timu inahitaji.

“Kila timu ina mwenyewe, ushindi wa Simba Chama akiwa kwenye ubora wake basi ujue hatufungwi kwa namna yoyote na timu yoyote,” .

SOMA NA HII  SIMBA YAWASHUSHIA AL AHLY BEI YA KUMPATA LUIS..SASA WANATAKA 650K TU