Ligi Kuu

NAMUNGO: TUKO TAYARI KUUWASHA MOTO SHINYANGA

admin March 3, 2021 9:47 am

KIKOSI cha klabu ya Namungo kimetamba kujipanga vizuri kwa ajili ya kuhakikisha wanaibuka na ushindi katika mchezo wao wa leo dhidi ya Mwadui.

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa katika dimba la Mwadui Complex, mkoani Shinyanga majira ya saa nane kamili mchana. 

Namungo wametamba kuwa, ushindi wa bao 1-0 walioupata siku ya Jumapili dhidi ya Mbeya City, katika michuano ya kombe la Shirikisho umezidi kuamsha ari ya kuhakikisha wanashinda mchezo wa leo. 

Akizungumzia maandalizi yao kuelekea mchezo huo, Ofisa habari wa Namungo, Kindama Namlia amesema: “Kikosi chetu kiliwasili salama mkoani Shinyanga jana kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo wetu dhidi ya kikosi cha Mwadui.

“Ushindi tulioupata katika mchezo uliopita dhidi ya Mbeya City kwenye michuano ya kombe la FA, umezidi kutupa ari ya kufanya vizuri kwenye mchezo huu wa Ligi Kuu,”

BAADA YA KUONGEZA MKATABA, KANGWA KUANZA NA POINTI ZA KAGERA SUGAR MAVITU YA DILUNGA YAMKUNA MFARANSA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply