epl

MANCHESTER UNITED WAPO TAYARI KUMSIKILIZA de GEA

admin March 10, 2021 5:47 am


 IMERIPOTIWA kuwa Klabu ya Manchester United imeanza mazungumzo na kipa wake namba moja David de Gea ili kumsikiliza ofa yake.

Ripoti zinaeleza kwamba United itamsikiliza kipa huyo kile anachokihitaji na itampa ruksa ya kufanya chaguo analotaka yeye bila kumbana kwa  kuwa amefanya nao kazi kwa ukaribu na muda mrefu.

Ikiwa David de Gea akaamua kasepa ndani ya kikosi hicho kinachonolewa na Ole Gunnar Solskjaer itakuwa ni nafasi kwa Dean Henderson kuwa kipa namba moja.

Tayari Ole Gunnar Solskjaer ameanza kumuamini kijana Henderson kikosi cha kwanza lengo ikiwa ni kumjengea hali ya kujiamini ili aweze kurithi mikoba ya de Gea ambaye ameanza kikosi cha kwanza kwenye jumla ya mechi 434.



SIMBA YATUPA KOMBORA KIMTINDO KWA YANGA, YAWAPA SOMO LA KUWAFIKIA WALIPO STARS YAANZA SAFARI YA AFCON

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply