Simba SC

MGOSI: ACHA KAZI IENDELEE

admin March 24, 2021 2:47 pm

 


LICHA ya kuwa katika majonzi makubwa kutokana na kuondokewa kwa Hayati Rais Dk John Pombe Magufuli, kikosi cha Simba Queens kimeendelea kujipanga vizuri kumalizia msimu wa Ligi Kuu ya Wanawake kwa kufanya mazoezi mara moja kwa siku.

Akizungumzia programu zao za mazoezi Mussa Mgosi amesema: “Kama Watanzania na kwa niaba ya Simba Queens niseme kuwa, tumeghubikwa na majonzi makubwa kwa kuondokewa na Rais John Pombe Magufuli.

“Na licha ya kuwa katika hali hii ya majonzi, bado tunaendelea kumuenzi Rais kwa sera yake kufanya kazi na kujituma kwa kuendelea na mazoezi ambayo kwa sasa tunafanya mara moja kwa siku kulinganisha na mara mbili ambazo tulikuwa tukifanya hapo mwanzo.”

YANGA KUJA KIVINGINE, WATAALAMU WASAUZ, LATVIA KUONGEZA NGUVU MKWASA ATAJA KILICHOIPOTEZA RUVU SHOOTING

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply