Home Taifa Stars EQUATORIAL YAIFUNGASHIA VIRAGO STARS AFCON

EQUATORIAL YAIFUNGASHIA VIRAGO STARS AFCON


 KUPOTEZA kwa timu ya Taifa ya Tanzania,  Taifa Stars mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu Afcon mbele ya Equatorial Guinea kumeifungashia jumla timu hiyo Kwenye michuano hiyo mikubwa Afrika. 


Stars ilikubali kichapo cha bao 1-0 ikiwa ugenini ndani ya kundi J na kuifanya ibaki na pointi zake 4 baada ya kucheza jumla ya mechi 5.


Equatorial Guinea wanafikisha pointi 9 zinazowafanya waungane na Tunisia wenye pointi 13 ambao wanaongoza kundi J na wemefuzu Afcon.


Timu ya Stars chini ya Kim Poulsen imepoteza mchezo wake tatu na ina mchezo mmoja wa kukamilisha ratiba dhidi ya Libya wenye pointi tatu.

SOMA NA HII  KOCHA WA TAIFA STARS ATEMA 'CHECHE' SAKATA LA MSUVA NA TIMU YAKE...AMPA SHARTI ZITO..LA SIVYO ...