Namungo FC

NAMUNGO FC YAREJEA BONGO, TAYARI KWA LIGI KUU BARA

admin April 12, 2021 10:47 am


 KIKOSI cha Namungo FC kinachonolewa na Kocha Mkuu, Hemed Moroco leo Aprili 12 kimerejea Tanzania kikitokea nchini Zambia ili kuendelea na mechi zake za Ligi Kuu Bara.

Namungo jana Aprili ilikuwa na kibarua cha kuipeperusha Tanzania kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Nkana FC.

Mchezo huo dakika 90 zilikamilika kwa Nkana FC kushinda bao 1-0 dhidi ya Namungo na kufanya kikosi hicho kilicho kwenye kundi D  kupoteza mechi zake mbili mbele ya Nkana FC.

Ule wa kwanza walipokutana Uwanja wa Mkapa, ubao ulisoma Namungo 0-2 Nkana FC. Kwenye kundi D Namungo FC ipo nafasi ya nne bado haijakusanya pointi.

Morocco amesema:”Tumeshawasili tayari Tanzania muda huu, tunamshukuru Mungu kwa kuwa tumerejea salama,” . 

MOURINHO ALIA NA VAR KISA KIWIKO CHA POGBA VIUNGO WAWILI WA MTIBWA SUGAR WAREJESHA MATUMAINI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply