Simba SC

KUMBE HATARI YA MORRISON NI KILA BAADA YA DAKIKA 118

admin May 4, 2021 7:47 am


 MZEE wa kukera ndani ya ardhi ya Bongo, Bernard Morrison ambaye ni mali ya Simba kwa sasa akitokea Klabu ya Yanga, hatari yake inaonyesha ni kila baada ya dakika 118.

 

Morrison amekuwa mzee wa matukio pia akiwa Simba ambapo aliwahi kukumbana na adhabu ya kufungiwa mechi tatu na Kamati ya Masaa 72 kwa kitendo cha kupigana na mchezaji wa Ruvu Shooting, Juma Nyoso wakati ubao wa Uwanja wa Uhuru ukisoma Simba 0-1 Ruvu Shooting.

 

Pia hivi karibuni kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Mwadui FC, Uwanja wa Kambarage wakati ubao ukisoma Mwadui 0-1 Simba, alionekana na hatia ya kumvuta mwamuzi msaidizi jambo lililopeleka apewe onyo na Kamati ya Masaa 72.

 

Kwenye ligi amecheza mechi 16, amefunga mabao matatu na pasi nne za mabao, ametumia dakika 832 na kumfanya ahusike kwenye jumla ya mabao 7 kati ya 58 ambayo yamefungwa na timu hiyo.

 

Mechi zake ilikuwa mbele ya:- Ihefu, dk 67, Mtibwa Sugar, dk 66, Biashara United, dk 25, Gwambina FC, dk 23, JKT Tanzania, dk 13, Prisons, dk 90, Ruvu Shooting, dk 45, Coastal Union, dk 90, Polisi Tanzania, dk 61.Dodoma Jiji, dk 70, Azam FC, dk 20, Biashara United, dk 80, Prisons, dk 24, Mwadui, dk 45, Gwambina, dk 62 na Dodoma Jiji dk 51

GUARDIOLA HAITAKUWA KAZI NYEPESI MBELE YA PSG YANGA: TUNA ASILIMIA KUBWA YA KUSHINDA MBELE YA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply