Yanga SC

NCHIMBI: KUFUNGA MBELE YA GWAMBINA FC KUMENIONGEZEA HALI YA KUJIAMINI

admin May 5, 2021 6:47 am


 NYOTA wa Yanga, Ditram Nchimbi ameweka wazi kuwa kufunga kwake bao mbele ya Gwambina FC kumemuongezea nguvu ya kuweza kujiamini zaidi kwa ajili ya mechi zinazofuata.

Mshambuliaji huyo mzawa hakufunga kwa muda wa mwaka mmoja jambo ambalo lilifanya mashabiki kumlalamikia kwamba hawezi kufunga.

Bao lake hilo alifunga mbele ya Gwambina FC, Uwanja wa Mkapa wakati wakishinda mabao 3-1.

Nchimbi ambaye kwenye mechi zote za Kariakoo Dabi za ligi amecheza anapewa nafasi ya kuanza katika mchezo ujao dhidi ya Simba, Mei 8.

Nyota huyo amesema:”Kufunga mbele ya Gwambina kwangu ni furaha na kunaongeza hali ya kujiamini kwa ajili ya mechi nyingine zijazo.

“Imani yangu ni kwamba ikiwa nitaendelea kupata nafasi itakuwa rahisi kwangu kufunga mabao mengi zaidi,” .

MAPILATO WA SIMBA V YANGA, WACHEZAJI WAJIANDAE KISAIKOLOJIA MZEE WA UTOPOLO ANAFUNGUKIA MECHI YA SIMBA V YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply