SHABIKI mkubwa wa Klabu ya Simba, Aggy ambaye amejichora nembo ya Simba kwenye mkono wake amesema kuwa aliamua kujiita Miss Simba kwa kuwa anaamini kwamba jina la Simba litabaki ila mchezaji anaweza kuondoka katika timu ambayo atakuwa hapo. Pia ameweka wazi kuwa familia yake ni familia ya mpira.