Simba SC

AJIBU ANAPATA TABU KWELI SIMBA KWA SASA

admin June 6, 2021 9:47 am

NYOTA wa Simba, kiungo Ibrahim Ajibu anapata tabu chini ya Kocha Mkuu, Didier Gomes kwa kujenga ushkaji mkubwa na benchi huku akishindwa kufikia rekodi yake ya msimu wa 2018/19 alipokuwa Yanga.
Nyota huyo alikuwa ni namba moja kwa kutengeneza pasi za mwisho Bongo, ambapo alitoa jumla ya pasi 17 ambazo hazijaweza kuvunjwa na nyota yoyote kwa sasa katika Ligi Kuu Bara.
Msimu huu akiwa ndani ya Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes ameshindwa kufurukuta kikosi cha kwanza kutokana na ushindani wa namba jambo ambalo limemfanya acheze jumla ya mechi 7.
Katika mechi hizo saba ni mechi tatu alianzia kikosi cha kwanza na nne akianzia benchi. Ametumia jumla ya dakika 236 akiwa ametupia bao moja na kutoa pasi moja ya bao.
Gomes amesema kuwa mchezaji atakayepata nafasi ya kuanza kikosi cha kwanza ni yule atakayefanya vizuri mazoezini.
Imekuwa ikitajwa kuwa nyota huyo msimu ujao atakuwa ndani ya kikosi chake cha zamani cha Yanga baada ya kupewa dili la miaka miwili.
Ikiwa dili hilo litakamilika atajiunga na timu hiyo bure kwa kuwa dili lake la miaka miwili linafika ukingoni msimu utakapomeguka.

OBREY CHIRWA AWAACHIA VIONGOZI HATMA YAKE NDANI YA AZAM FC AZAM FC YA LWANDAMINA YAPIGA PINI MABAO 28

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply