Azam FC

AZAM FC KAMILI KWA AJILI YA NAMUNGO FC

admin June 20, 2021 8:47 am


UONGOZI wa Azam FC umeweka wazi kwamba upo tayari kwa ajili ya mchezo wao wa ligi dhidi ya Namungo FC utakaochezwa kesho, Uwanja wa Majaliwa.

Azam FC inayonolewa na Kocha Mkuu, George Lwandamina ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 63 baada ya kucheza jumla ya mechi 31.

Mchezo wa kwanza walipokutana Uwanja wa Azam Complex ubao ulisoma Azam FC 2-2 Namungo hivyo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Zakaria Thabit, Ofisa Habari wa Azam FC amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mechi zote zijazo hivyo watapambana kupata pointi tatu. 

Ikumbukwe kwamba Azam FC imetoka kushinda kwa mabao 4-1 dhidi ya Gwambina FC kwenye mchezowa ligi uliochezwa Uwanja wa Azam Complex.

Mpiana Monzizi na Idd Seleman nyota hawa walitupia mabao mawilimawili kila mmoja.

RAMANI YA USAJILI YANGA YACHORWA NAMNA HII VIDEO: METACHA MNATA HAJALIPWA YANGA, ISHU YAKE SIMBA MENEJA AFUNGUKA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply