CAF

KAIZER CHIEFS YAWAPA TABU WAYDAD LIGI YA MABINGWA AFRIKA

admin June 20, 2021 2:47 pm

 SAMIR Nurkovic nyota wa kikosi cha Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini alifunga bao pekee la ushindi katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wydad AC.

Katika mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Mohammed V, Wydad waliutawala mchezo kwa asilimia 79 huku Kaizer Chiefs ambao walikuwa ugenini walikuwa na asilimia 21.

Ilikuwa dakika ya 34, Samir alipachika bao hilo na kufanya timu yao ipige jumla ya mashuti matatu huku lililolenga lango likiwa moja lililojaa wavuni.

Wydad wao walipiga jumla ya mashuti 28 na ni 8 yalilenga lango na katika pasi Wydad walipiga jumla 670 huku Kaizer Chiefs ambao walizima ndoto za Simba kutinga hatua ya nusu fainali walipiga pasi 183.

Mtanzania Simon Msuva alianzia benchi na hata alipoingia ngoma ilikuwa nzito.

KASEKE, FEI TOTO WAWEKA REKODI YAO KWA MKAPA KIKOSI CHA YANGA KITAKACHOANZA LEO DHIDI YA MWADUI FC

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply