Simba SC

KUHUSU WANAOSAJILI KUJA KUCHEZA NAMBA YAKE..ZIMBWE JR AMEFUNGUKA HAYA

admin June 20, 2021 7:37 am


SIMBA kwa misimu mitatu tofauti imekuwa ikisajili beki wa kushoto wa kumpa ushindani beki wao wa sasa aliyejimilikisha namba kikosi cha kwanza, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ na kwa sasa anatafutwa beki mwingine, lakini mwenyewe amesema wala hana presha yeyote.

Tshabalala, amesema kuwa, wachezaji hao ambao wamekuwa wakisajiliwa katika nafasi hiyo wamekuwa ni chachu zaidi ya kukua kwa kiwango chake kwani kadri apatavyo ushindani ndivyo anavyozidi kujibidiisha ili awe imara zaidi kuepuka kupoteza namba.

Alisema huwa anafurahia kupata changamoto na ushindani kwa vile humfanya asibweteke kama ambavyo angekuwa mwenyewe katika nafasi hiyo na kubwa kwake ni kutaka kuendelea kubaki kikosi cha kwanza.

“Kama unakumbuka katika mechi ya mwisho msimu uliopita dhidi ya Mtibwa Sugar tulipochukua taji nilieleza msimu huu tunatetea tena ubingwa na tunakwenda kulitimiza hilo, hivyo kiu hii ya kutaka kuona inapata matokeo mazuri ndio inayonifanya nijitume zaidi mazoezi na uwanjani,” alisema Tshabalala.

Kwa misimu mitatu Simba imesajili mabeki wa kushoto akiwamo Asante Kwasi, Jamal Mwambeleko na Gadiel Michael ambao wote wameshindwa kufua dafu mbele yake Tshabalala na kwa sasa inaeleza mabosi wa klabu hiyo wanaendelea kusaka mwingine wa kuwaongeza nguvu.

MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA UPO NAMNA HII KWA SASA RAMANI YA USAJILI YANGA YACHORWA NAMNA HII

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply