EURO 2020

DAEI AMPONGEZA RONALDO KWA KUFIKIA REKODI YAKE YA MABAO 109

admin June 24, 2021 1:47 pm


MSHAMBULIAJI wa zamani wa timu ya Taifa ya Irani, Ali Daei amempongeza mshambuliaji na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno, Cristiamo Ronaldo kufuatia nyota huyo kufikia rekodi ya mabao 109 katika michezo ya kimataifa.

Ronaldo alifikia rekodi hiyo baada ya kufunga mabao mawili kwa mikwaju ya penalti katika mchezo wao wa jana dhidi ya Ufaransa.

Daei aliwasilisha pongezi hizo kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram ambapo ameandika: “Hongera sana Cristiano ambaye sasa umebakiza bao moja kuvunja rekodi ya kufunga mabao kwa wanaume kimataifa.

“Ni heshima kubwa kwamba mafanikio haya kwa sasa yatakuwa ya Ronaldo bingwa mkubwa wa soka, na binadamu anayejali ambaye pia huchochea huwapa moyo wengine.”

MOTO WA SALAH LIGI KUU ENGLAND NI BALAA BREAKING: MWAKALEBELA ASHINDA KESI YAKE TFF

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply