Home EURO 2020 UKRAINE YATINGA ROBO FAINALI EURO 2020

UKRAINE YATINGA ROBO FAINALI EURO 2020


 KATIKA mchezo wa hatua ya 16 bora hatimaye Ukraine imetinga hatua ya robo fainali kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Sweden.


Ni Oleksandr Zinchenko dk 27 alifungua pazia la ushindi kwa Ukraine likawekwa usawa na Emil Forsberg.


Mpaka dk 90 zinakamilika ubao wa Uwanja wa Hampden Park ulikuwa unasoma Sweden 1-1 Ukraine.


Kwenye dk 30 zs nyongeza ni Artem Dovbyk alipachika bao dk 120+1 na kuifanya timu yake ya Taifa ya Ukraine kutinga hatua ya robo fainali.


Ni Marcus Danielson dk 99 alionyeshwa kadi nyekundu na kuwafanya Sweden kumaliza pambano hilo la Euro 2020 wakiwa pungufu.

SOMA NA HII  UFARANSA YAFUNGUA EURO 2020 KWA USHINDI, POGBA NYOTA WA MCHEZO