KMC FC

KMC WAFUNGUKIA ISHU YA KUMKODI MZEE MPILI

admin July 7, 2021 8:47 am

WAKATI leo Julai 7 Klabu ya KMC ikitarajiwa kusaka pointi tatu mbele ya Simba, mabosi wa timu hiyo wamefungukia ishu ya kudaiwa kumkodi Haji Omari Mpili, maarufu kama Mzee Mpili.
Jana, Julai 6 ilisambaa twiter iliyokuwa inaonesha kwamba inamilikiwa na Klabu ya KCM ambayo ilisomekana namna hii:”Tumemkodi kwa muda Mzee Mpili, mtajua amjui,”.
Akizungumza na Championi Jumatano, Ofisa Habari wa KMC, Christina Mwagala alisema kuwa akaunti hiyo sio yao na wala hawana mpango wa kufanya hivyo.
“Hiyo akaunti siyo yetu na hatuijuia kabisa kwa kweli, hatuna mpango wa kufanya hivyo vijana wetu wapo vizuri na maandalizi yapo sawa,” .
Mzee Mpili amekuwa akitamba kwamba ushindi wa Yanga walioupata Julai 3 wa bao 1-0 dhidi ya Simba ni yeye alikuwa mchezaji namba moja jambo ambalo lilifanya KMC wadai kwamba nao watamkodi kwa muda.
Mpili alisikika akisema kuwa:”Ushindi wa Yanga mimi nilikuwa mchezaji namba moja hivyo hakukuwa na namna kwa Simba kutufunga ilikuwa lazima wafungwe kwa kuwa mimi nina watu,” .

 

KATWILA: TUTAFANYA VIZURI KWENYE MECHI ZETU WACHEZAJI YANGA WAPEWA MINOTI KISA KUIMALIZA SIMBA KWA MKAPA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply