Simba SC

CHUKI ZA BARBRA ZAMPA HOFU HAJI MANARA

admin July 22, 2021 7:47 am

 HAJI Manara, Ofisa Habari wa Simba amesema kuwa anahofia kula chakula akiwa mbele ya Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez kutokana na kile anachodai ni chuki kali aliyonayo kiongozi huyo.

Kupitia sauti ambayo imekuwa ikisambaa kwenye mitandao sauti ya mtu anayesadikika kuwa ni Manara imesikika ikisema kwamba miongoni mwa vitu ambavyo vinampa shida ndani ya Simba ni roho ya chuki.

“Barbra wewe una chuki na roho mbaya sijawahi kuona mpaka naogopa kula chakula mbele yako. Umekuwa ukiwadhalilisha wafanyakazi wa Simba jambo ambalo ni baya,” ilisikika sauti hiyo.

Pia habari zinaeleza kuwa Manara anampango wa kubwaga manyanga Simba mara baada ya fainali Kigoma Julai 25 ambapo itakuwa ni Yanga v Simba, Uwanja wa Lake Tanganyika,  Kombe la Shirikisho.

YANGA WATIA TIMU KIGOMA MAPEMA KUIWAHI SIMBA MBUNGE SHANGAZI ATEULIWA KUMRITHI BARBARA NDANI YA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply