Yanga SC

FEI TOTO: MAMBO MAZURI YANAKUJA MSIMU UJAO

admin July 29, 2021 1:46 pm


BAADA ya kukosa ubingwa wa Ligi Kuu Bara na Kombe la FA, Kiungo mshambuliaji wa Yanga Feisali Salum ‘Fei Toto’ amefunguka na kuwataka mashabiki wa timu hiyo kutokata tamaa kwani wanaenda kujipanga ili kufanya vizuri msimu ujao.

Katika  msimu huu wa Ligi Kuu Bara alifanikiwa kuifungia timu yake ya Yanga   mabao matano na kutoa pasi moja ya bao.

Akizungumzia mipango yao, Feitoto amesema kuwa mashabiki wa timu yao wasikate tama kwani mambo mazuri yanakuja msimu ujao wanaendelea kujipanaga kurejesha furaha ya mashabiki wao.

“Tunawaomba mashabiki  wetu  wasikate tama  kwani mambo mazuri yanakuja waendelee kuwa pamoja na sisi, na tunawashukuru sana kwa sapoti wanayotuonyesha na tunawaahidi kufanya vizuri msimu ujao.

“Msimu huu hatujafanikiwa kufikia malengo yetu lakini hatuja kata tama tunaendelea kujipanaga ili kuhakikisha tunafanya vizuri zaidi na kutimiza malengo yetu,”amesema Feisal.

VIDEO: SVEN KUMCHOMOA CHAMA NDANI YA SIMBA, KAIZER WATIA MKONO, SIMBA WAFUNGUKA AZAM FC WAANIKA MIPANGO YAO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply