KMC FC

KINACHOWASUBIRISHA KMC WASHINDWE KUSAJILI HIKI HAPA

admin August 12, 2021 12:44 pm


 UONGOZI wa Klabu ya KMC iliyomaliza ligi ikiwa nafasi ya tano na pointi 48 baada ya kucheza mechi 34 umebainisha kwamba utakamilisha usajili wa majembe ya kazi utakapopata ripoti.

Dirisha la usajili likiwa limefunguliwa tayari timu zimeanza kuingia sokoni kusaka nyota wapya ambao watafanya kazi na timu zao ila kwa KMC wao bado hawajaanza vurugu zao.

Ofisa Habari wa KMC wazee wa pira kodi, Christina Mwagala amesema kuwa wanatambua ni wakati wa usajili lakini watafanya kazi pale watakapopokea ripoti.

“Kwa sasa tupo na tunaendelea kufanya kazi imekuwa ni kawaida yetu kila wakati wa usajili kuwa kimya bila vurugu lakini mwisho wa siku tunafanya usajili mzuri.

“Kinachosubiriwa wakati huu ni ripoti ya mwalimu, hatuwezi kusajili bila kutumia ripoti ambayo kwa sasa bado hatujakabidhiwa ikiwa tayari kila kitu kitafanyika,” amesema Christina.

METACHA AFUNGUKA ISHU YA KUPIGWA CHINI YANGA VIDEO: SIMBA YATUA KWA KIUNGO WA MALI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply