Simba SC
SIMBA YAMCHOMOA MWINGINE KAGERA SUGAR, AJIFUNGA MIAKA MITATU
NYOTA Abdul Swamad leo Agosti 17 ametambulishwa kuwa mali ya Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes.
Nyota huyo anayecheza pia timu ya taifa ya Zanzibar Heroes alikuwa anakipiga ndani ya Kagera Sugar.
Anakuwa nyota wa pili kusaini Simba akitokea Mtibwa Sugar baada ya Yusuph Mhilu naye ambaye alikuwa anacheza Kagera Sugar kusaini.
Wote wawili wamesaini dili la miaka mitatu kuitumikia timu hiyo ambayo imeweka kambi Morocco.

Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.