Home Yanga SC BAADA YA KUACHWA NA YANGA..JUMA MAKAPU AFUNGUKA HAYA..AWATAJA VIONGOZI

BAADA YA KUACHWA NA YANGA..JUMA MAKAPU AFUNGUKA HAYA..AWATAJA VIONGOZI


Hatimaye Klabu ya Young Africans imeachana na Kiungo Said Juma Makapu katika usajili wa kuelekea msimu mpya wa 2021/22.

Hatua ya kuachwa kwa kiungo huyo, imefahamika baada ya Makapu kuandika maneno ya kuwaaga Mashabikj na Wanachama wa Young Africans kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Makapu ameandika: “Hakika ilikuwa ni miaka 7 bora Sana kwangu, ndani na nje ya Uwanja. Yanga ilikuwa sehemu ya familia Yangu.

Nitoe Shukrani zangu za dhati kwa Uongozi, benchi la Ufundi, wachezaji na mashabiki wote, kwa kuniamini na kuniunga mkono katika kila Jambo”

“Ni mengi nimejifunza na nina amini yatanisaidia kunijenga zaidi Kama mchezaji. asanteni sana. Wakati mwingine tena, Wananchi,”

Said Juma Makapu.

SOMA NA HII  PAMOJA NA KUWA KILELENI...UONGOZI YANGA WAIBUKA A HILI JIPYA..WAIBANA SIMBA KISAWASAWA...