BAADA ya jana Agosti 24 Haji Manara aliyekuwa Ofisa Habari wa Simba kutambulishwa ndani ya Yanga kazi yake ya kwanza ilikuwa ni ya uzinduzi wa uzi mpya utakaotumika na timu hiyo kwa msimu wa 2021/22.
Inakuwa ni kazi yake ya kwanza kuifanya baada ya kutambulishwa ndani ya kikosi cha Yanga na Senzo Mbatha ambaye ni Mshauri Mkuu kuelekea katika mabadiliko ya timu.