Home Yanga SC YANGA KUSHUSHA NYOTA WENGINE WAWILI WA KIMATAIFA

YANGA KUSHUSHA NYOTA WENGINE WAWILI WA KIMATAIFA


UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kwamba zoezi la usajili bado linaendelea kukamilisha masuala ya usajili.

Kwa sasa ikiwa ni dirisha la usajili tayari nyota kadhaa wameshatambulishwa Yanga ikiwa ni pamoja na Heritier Makambo, Fiston Mayele, Dickson Ambundo.

Timu hiyo pia inatarajia kuelekea nchini Morocco kwa ajili ya kuweka kambi kwa muda ikiwa ni maandalizi ya msimu wa 2021/22.

“Usajili wengi wanadhani kwamba ni kuwatangaza wachezaji ila kuna vitu vingi ikiwa kupata vibali vyao, kusaini mkataba, kuwaingiza kwenye mfumo na vitu kama hivyo sisi vyote tunakwenda navyo sambamba.

“Ili aweze kusajiliwa lazima awe amekamilisha kila kitu kuanzia usajili. Bado hatujamaliza usajili. Kuna wachezaji wawili wakubwa wa kimataifa ambao tutawasijili.Hivyo mashabaki watulie wasubiri hivi karibuni watatambulishwa,” .

SOMA NA HII  YANGA YATEMBEZA MKWARA,KUISIMAMISHA NCHI NA AFRIKA...WATAMBIA USAJILI BORA