Home news BAADA YA KUMUONA MAYELE AKICHEZA …MWINYI ZAHERA AGUNA KISHA AKAFUGUKA HAYA..

BAADA YA KUMUONA MAYELE AKICHEZA …MWINYI ZAHERA AGUNA KISHA AKAFUGUKA HAYA..


KOCHA wa zamani wa Yanga, Mwinyi Zahera juzi alitinga kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa akishuhudia Tamasha la timu hiyo la Wiki ya Mwananchi ambalo liliambatana na mechi ya kirafiki kati ya Yanga na Zanaco kutoka Zambia.

Zahera ambaye ni raia wa DR Congo, alishuhudia kila kitu na baada ya mechi alipiga stori na  na kufunguka alichokiona huku akimtaja Fiston Mayele kama mshambuliaji hatari zaidi.

Kocha huyo alisema kuwa anawajua Watanzania wanapenda vitu vipya, hivyo kwa mechi ya juzi pekee haiwezi kuwafanya wamkubali haraka Mayele lakini akianza kucheza mechi za ushindani watamkoma.

“Naijua Yanga, nawajua vyema mashabiki wa timu hii pia namjua Mayele. Kwa leo hajaonekana kufanya kitu kikubwa kutokana na muda lakini subirini acheze kisha mtakuja kunieleza ninayowaambia. Mayele ni mshambuliaji kweli kweli,” alisema Zahera ambaye hakutaka kuweka wazi kwamba ana dili gani kwasasa Dar es Salaam licha ya kwamba awali aliwahi kuhusishwa na skauti ya Simba mpya.

Sambamba na kumsifia Mayele, Zahera alizungumzia kikosi kizima cha Yanga kwa kusema wana wachezaji wazuri hivyo kilichobaki ni kazi kwa kocha tu.

“Timu ina Makambo, Mayele, Moloko na washambuliaji wengine ambao ni hatari, pia ina viungo na mabeki wazuri, hapa kazi ni kwa kocha kuijenga timu yenye kueleweka kwani kwa mchezaji mmoja kila mtu ana uwezo mkubwa,” alisema Zahera.

Zahera alitua Yanga msimu wa 2017/2018.

SOMA NA HII  KUELEKEA MECHI DHIDI YA AZAM..'FEI TOTO' ASHINDWA KUJIZUIA...AANIKA MAPENZI YAKE HADHARANI...