Home news SIMBA YAJA NA SLOGAN MPYA,VIINGILIO VYATAJWA

SIMBA YAJA NA SLOGAN MPYA,VIINGILIO VYATAJWA


KLABU ya Simba SC, Ezekiel Kimwaga leo Septemba 3, 2021amesema kuwa kuelekea katika Simba Day inayotarajiwa kufanyika Septemba 19 wanakuja na slogan mpya itakayotumika pamoja na viingilio.


Kamwaga  ameongea na Wanahabari katika mkutano uliofanyika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.

Kimwaga, ametangaza bei za viingilio kwenye Simba Day itakayofanyika mwezi huu Septemba 19, katika Uwanja wa Mkapa jijini Dar.

 

Kwa upande wa Platinum Tsh. 200,000, VIP Tsh 30,000, VIP B&C Tsh 20,000 na mzunguko ni Tsh 5,000.


“Slogan ya Simba Day 2021 ni One Team, One Dream tukimaliza na Asubuhi Tu, Twendeni Wenye Nchi.


“Maandalizi yapo vizuri na kwa sasa niwaombe mashabiki nguvu na macho yote tuelekeze kwenye tamasha letu ambalo litakuwa ni nzuri,” .

SOMA NA HII  KUMBE LWANGA SIMBA BADO SANA