KUPOTEZA kwa Simba kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya TP Mazembe jana Uwanja wa Mkapa kwenye tamasha la Simba Day, shabiki wa Yanga ameweka wazi kuwa kufungwa kwao ni uzembe wao kwa kuwa walipata muda mwingi wa kujiandaa tofauti na TP Mazembe.
Pia ameweka wazi pia timu ya Yanga kutolewa katika hatua ya awali ya Ligi ya mabingwa Afrika ni jambo ambalo linawaumiza ila inabidi wajipange.