BASI jipya la kisasa la Azam FC kwa sasa lipo Mbeya taratibu likiwa njiani kuibukia Dar es Salaam.
Ndinga hiyo mpya ambayo ni moja ya basi matata ni kwa ajili ya matumizi ya timu hiyo inayonolewa na Kocha Mkuu, George Lwandamina kwa msimu mpya wa 2021/22.
Inaitwa Mercedes Benz Irizar i6S Plus itafanya ziara kwenye mikoa mbalimbali kwa mwendo wa taratibu ili mashabiki waweze kuiona ndinga hiyo mpya.