Home news RT YAOMBA WADHAMINI WAJITOKEZE

RT YAOMBA WADHAMINI WAJITOKEZE


 CHAMA cha Riadha Tanzania (RT), kwa sasa ki
naendelea vizuri na mazoezi kuelekea mashindano ya riadha ya kitaifa yatakayofanyika Arusha, Oktoba 8 na 9, mwaka huu.

Licha ya kwamba wanaendelea vizuri bado wana tatizo la kukosa udhamini katika mashindano hayo jambo.

Akizungumza na Championi Ijumaa, Katibu Mkuu wa RT, Jackson Ndaweka, alisema kuwa wanahitaji kufanya vizuri kwenye hayo mashindano hivyo wadhamani wajitokeze kwa wingi kuwa bega kwa bega nao katika mashindano hayo.

“Mpaka sasa tuna wadhamini wawili tu ambao wameungana na sisi katika michezo ya riadha ambao ni CRDB na Azam TV, hivyo bado wadhamini ni changamoto kubwa kwetu katika kuendeleza riadha na mashindano kwa ujumla.”


SOMA NA HII  TRY AGAINI APIGILIA NYUNDO ISHU YA USAJILI SIMBA..ATAJA VYUMA VINNE VIPYAA...ADAI SIMBA NI KUBWA..